Swali: Nitaenda kumposa mwanamke na nauliza kama nalazimika kumweleza kwamba niliwahi kuoa hapo kabla?

Jibu: Kuna haja gani ya kumweleza kuwa uliwahi kuoa hapo kabla? Unakusudia uko na mke? Kama umeoa na hajui jambo hilo, unatakiwa kumbainishia. Hata hivyo hakuna haja ya kumweleza kwamba hapo kabla uliwahi kuoa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (29)
  • Imechapishwa: 11/02/2022