Swali: Ni ipi hukumu ya kuswali ndani ya chumba ambacho mna picha au sanamu kinyago cha wanyama au mtu kwa ajili ya mapambo?
Jibu: Ni haramu kuhifadhi picha na masanamu vinyago na kuyaweka ndani ya nyumba. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Usiache picha isipokuwa umeiharibu wala kaburi lililoinuliwa isipokuwa umelisawazisha.”
Amesema vilevile (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Malaika hawaingii ndani ya nyumba ambayo ndani mna mbwa au picha.”
Inachukiza kuswali ndani ya chumba kilicho na picha iliyoning´inizwa au iliyosimikwa na khaswa ikiwa upande wa Qiblah cha mswaliji. Lakini hata hivo swalah ni sahihi.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah bin Ghudayyaan
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalus-Shaykh
Bakr Abu Zayd
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (16147)
- Imechapishwa: 14/05/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket