Swali: Ni ipi hukumu ya kuswali ndani ya chumba ambacho mna picha au sanamu kinyago cha wanyama au mtu kwa ajili ya mapambo?
Jibu: Ni haramu kuhifadhi picha na masanamu vinyago na kuyaweka ndani ya nyumba. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Usiache picha isipokuwa umeiharibu wala kaburi lililoinuliwa isipokuwa umelisawazisha.”
Amesema vilevile (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Malaika hawaingii ndani ya nyumba ambayo ndani mna mbwa au picha.”
Inachukiza kuswali ndani ya chumba kilicho na picha iliyoning´inizwa au iliyosimikwa na khaswa ikiwa upande wa Qiblah cha mswaliji. Lakini hata hivo swalah ni sahihi.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah bin Ghudayyaan
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalus-Shaykh
Bakr Abu Zayd
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (16147)
- Imechapishwa: 14/05/2022
Swali: Ni ipi hukumu ya kuswali ndani ya chumba ambacho mna picha au sanamu kinyago cha wanyama au mtu kwa ajili ya mapambo?
Jibu: Ni haramu kuhifadhi picha na masanamu vinyago na kuyaweka ndani ya nyumba. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Usiache picha isipokuwa umeiharibu wala kaburi lililoinuliwa isipokuwa umelisawazisha.”
Amesema vilevile (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Malaika hawaingii ndani ya nyumba ambayo ndani mna mbwa au picha.”
Inachukiza kuswali ndani ya chumba kilicho na picha iliyoning´inizwa au iliyosimikwa na khaswa ikiwa upande wa Qiblah cha mswaliji. Lakini hata hivo swalah ni sahihi.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah bin Ghudayyaan
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalus-Shaykh
Bakr Abu Zayd
Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (16147)
Imechapishwa: 14/05/2022
https://firqatunnajia.com/swalah-ndani-ya-chumba-kilicho-na-picha-au-sanamu-kinyago/