Swali: Nini maana ya Hadiyth isemayo:
“Rak´ah mbili kwa kutumia Siwaak ni bora kuliko Rak´ah sabini pasi na kutumia Siwaak.”?
Jibu: Kutumia Siwaak kunapendeza wakati mtu anataka kuswali na wakati wa kutawadha. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Siwaak inasafisha mdomo na inamridhisha Mola.”[1]
Ameipokea an-Nasaa´iy kwa cheni ya wapokezi Swahiyh kutoka kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa).
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) tena:
“Lau nisingechelea kuwatia uzito ummah wangu basi ningeliwaamrisha kutumia Siwaak wakati wa kila swalah.”[2]
Kuna maafikiano juu ya usahihi wake.
Imekuja katika tamko lingine:
“Lau nisingechelea kuwatia uzito ummah wangu basi ningeliwaamrisha kutumia Siwaak wakati wa kila wudhuu´.”[3]
Ameipokea Imaam an-Nasaa´iy kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.
Kuhusu Hadiyth isemayo:
“Swalah ambayo mtu ametumia Siwaak ni bora kuliko swalah ambayo mtu hakutumia Siwaak.”
ni dhaifu na si Swahiyh. Yaliyopo katika Hadiyth Swahiyh yanatosheleza kutoihitajia.
[1] an-Nasaa´iy (05).
[2] al-Bukhaariy (887) na Muslim (252).
[3] an-Nasaa´iy (02/30430).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (26/29) https://binbaz.org.sa/fatwas/20197/فضل-السواك
- Imechapishwa: 23/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)