Swali: Du´aa ya kufungulia swalah imewekwa katika Shari´ah kuisoma katika swalah ya jeneza? Je, mtu alete Isti´aadhah kabla ya kuanza kisomo?
Jibu: Wanachuoni wamesema kuwa haikupendekezwa na wakasema ni kwa sababu ya kwamba swalah ya jeneza imejengwa juu ya ukhafifishaji. Ikiwa imejengwa juu ya ukhafifishaji basi kutakuwa hakuna du´aa ya kufungulia swalah.
Kuhusu kuleta Isti´aadhah afanye hivo kwa kuwa atasoma Qur-aan. Allaah (Ta´ala) amesema:
فَإِذَا قَرَأْتَ الْقُرْآنَ فَاسْتَعِذْ بِاللَّـهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ
“Unapotaka kusoma Qur-aan basi, omba ulinzi kwa Allaah kutokamana na shaytwaan aliyefukuzwa mbali.”[1]
[1] 16:98
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/119)
- Imechapishwa: 07/09/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket