Swali: Baada ya kumzika maiti kuna Hadiyth ya kwamba mtu abaki karibu na kaburi la yule maiti kwa kiasi cha muda wa kumchinja ngamia. Hilo lina maana gani?
Jibu: Haya aliusia ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh). Alisema:
“Baada ya kuzikwa simameni karibu na kaburi langu kwa kiasi cha muda wa kumchinja ngamia na kuigawa nyama yake.”[1]
Lakini Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwaamrisha Ummah wafanye hivo. Wala hayakufanywa na Maswahabah kutokana na ninavyojua. Pindi Mtume alipokuwa akimaliza kumzika maiti anasimama pembezoni naye na kusema:
“Muombeeni msamaha ndugu yenu na mumtakie uthabiti. Hakika hivi sasa ataulizwa.”[2]
Simama karibu na kaburi lake useme:
“Ee Allaah mthibitishe! Ee Allaah mthibitishe! Ee Allaah mthibitishe! Ee Allaah msamehe! Ee Allaah msamehe! Ee Allaah msamehe!”
Baada ya hapo wanaenda. Kubaki pale ni jambo halikuwekwa katika Shari´ah.
[1] Muslim (121).
[2] Abu Daawuud (3221).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/218)
- Imechapishwa: 26/08/2021
Swali: Baada ya kumzika maiti kuna Hadiyth ya kwamba mtu abaki karibu na kaburi la yule maiti kwa kiasi cha muda wa kumchinja ngamia. Hilo lina maana gani?
Jibu: Haya aliusia ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh). Alisema:
“Baada ya kuzikwa simameni karibu na kaburi langu kwa kiasi cha muda wa kumchinja ngamia na kuigawa nyama yake.”[1]
Lakini Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwaamrisha Ummah wafanye hivo. Wala hayakufanywa na Maswahabah kutokana na ninavyojua. Pindi Mtume alipokuwa akimaliza kumzika maiti anasimama pembezoni naye na kusema:
“Muombeeni msamaha ndugu yenu na mumtakie uthabiti. Hakika hivi sasa ataulizwa.”[2]
Simama karibu na kaburi lake useme:
“Ee Allaah mthibitishe! Ee Allaah mthibitishe! Ee Allaah mthibitishe! Ee Allaah msamehe! Ee Allaah msamehe! Ee Allaah msamehe!”
Baada ya hapo wanaenda. Kubaki pale ni jambo halikuwekwa katika Shari´ah.
[1] Muslim (121).
[2] Abu Daawuud (3221).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/218)
Imechapishwa: 26/08/2021
https://firqatunnajia.com/ni-muda-kiasi-gani-inatakiwa-kubaki-makaburini-baada-ya-mazishi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)