Swali: Ni ipi hukumu ya kumswalia maiti makaburini kwa yule ambaye hakumswalia?
Jibu: Sijui Sunnah yoyote juu ya hilo kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wala kutoka kwa Maswahabah. Lakini linaingia katika jumla ya makokotezo ya kumswalia maiti. Mtu anaweza kutumia hilo dalili vilevile kwa kitendo cha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pindi aliposwalia kaburi la mwanamke aliyekuwa akifuagia msikiti.
Mtu akija ilihali ameshapitwa na swalah msikitini amswalie na haina neno. Anapata ujira – Allaah akitaka.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/140)
- Imechapishwa: 15/09/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket