Swali: Ni ipi hukumu ya kusoma Qur-aan tukufu kwa maiti na kuweka msahafu juu ya tumbo lake? Kutoa pole kuna kikomo cha idadi ya masiku? Inasemekana kuwa ni siku tatu.
Jibu: Hakuna asli sahihi juu ya kumsomea Qur-aan maiti na kusoma karibu na kaburi la yule maiti. Sio jambo limewekwa katika Shari´ah. Bali ni Bid´ah.
Kadhalika kuweka msahafu juu ya tumbo lake ni jambo halina asli. Halikuwekwa katika Shari´ah. Walichosema baadhi ya wanachuoni ni kwamba kuwekwe kipande kidogo cha chuma au kitu kizito juu ya tumbo la maiti ili lisivimbe.
Kuhusu kutoa pole, hakuna kikomo cha masiku kadhaa.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/216)
- Imechapishwa: 25/08/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket