Swali: Tunaona namna ambavo baadhi ya watu wanaweka upande mmoja wa kaburi la maiti alama ya simenti ambayo wanaandika juu yake jina la maiti na tarehe ya kufariki kwake na wakati mwingine wanaweza kunyanyua jengo lake.
Jibu: Haya yamekatazwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kuandika juu ya kaburi[1]. Baadhi ya wanazuoni wameruhusu kuweka alama au jina peke yake.
Kuhusu kuandika tarehe ya kufariki kwake, jina la baba yake, jina la babu na mfano wake au kukaandikwa baadhi ya Aayah za Qur-aan ni miongoni mwa Bid´ah ambazo zinatakiwa kuondoshwa na kubadilishwe jiwe kwa jingine. Aidha jiwe linalowekwa halitakiwi kunyanyuliwa ziadi kuliko makaburi mengine. Jiwe hilo linatakiwa liwe sawa na mawe mengine. Kwa sababu ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) alisema kumwambia Abul-Hayyaaj al-Asadiy:
“Hivi nisikutume juu ya kazi aliyonituma kwayo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)? Usiache picha hata moja isipokuwa umeiharibu wala kaburi lililoinuka isipokuwa umelisawazisha.”[2]
[1] at-Tirmidhiy (1052) ambaye amesema kuwa ni nzuri na Swahiyh.
[2] Muslim (969).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/190-191)
- Imechapishwa: 24/05/2022
Swali: Tunaona namna ambavo baadhi ya watu wanaweka upande mmoja wa kaburi la maiti alama ya simenti ambayo wanaandika juu yake jina la maiti na tarehe ya kufariki kwake na wakati mwingine wanaweza kunyanyua jengo lake.
Jibu: Haya yamekatazwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kuandika juu ya kaburi[1]. Baadhi ya wanazuoni wameruhusu kuweka alama au jina peke yake.
Kuhusu kuandika tarehe ya kufariki kwake, jina la baba yake, jina la babu na mfano wake au kukaandikwa baadhi ya Aayah za Qur-aan ni miongoni mwa Bid´ah ambazo zinatakiwa kuondoshwa na kubadilishwe jiwe kwa jingine. Aidha jiwe linalowekwa halitakiwi kunyanyuliwa ziadi kuliko makaburi mengine. Jiwe hilo linatakiwa liwe sawa na mawe mengine. Kwa sababu ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) alisema kumwambia Abul-Hayyaaj al-Asadiy:
“Hivi nisikutume juu ya kazi aliyonituma kwayo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)? Usiache picha hata moja isipokuwa umeiharibu wala kaburi lililoinuka isipokuwa umelisawazisha.”[2]
[1] at-Tirmidhiy (1052) ambaye amesema kuwa ni nzuri na Swahiyh.
[2] Muslim (969).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/190-191)
Imechapishwa: 24/05/2022
https://firqatunnajia.com/ni-ipi-hukumu-ya-kuandika-jina-la-maiti-na-tarehe-ya-kufa-kwake-juu-ya-jiwe-la-kaburi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)