Swali: Je, inafaa kwa mwanamke mwenye hedhi na mwenye damu ya uzazi kugusa Qur-aan na kusoma ndani yake khaswa katika mwezi wa Ramadhaan wenye baraka ambao watu wanapupia kukhitimisha Qur-aan?
Jibu: Sijui kizuizi juu ya hilo. Hadiyth isemayo:
“Haigusi Qur-aan isipokuwa aliye msafi.”
Wako wanaosema kuwa kuna Swahabah anayekosekana katika cheni ya wapoezi. Tukikadiria kuwa ni nzuri kwa mkusanyiko wa njia zake inafasiriwa kama alivosema ash-Shawkaaniy katika “Nayl-ul-Awtwaar”:
“Haigusi Qur-aan isipokuwa aliye msafi.”
“Maana yake ni muislamu.”
Kwa maana nyingine haigusi ambaye ni kafiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza mtu kusafiri na Qur-aan kwenda katika miji ya maadui.
Kuhusu maneno Yake (Ta´ala):
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
“Hawaigusi isipokuwa waliotwahara.”[1]
Kinachokusudiwa ni Malaika. Hivo ndivo amesema Imaam Maalik katika “al-Muwattwa´”. Akaongezea kwamba Aayah hiyo inafasiriwa na maneno Yake (Ta´ala):
كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ بِأَيْدِي سَفَرَةٍ كِرَامٍ بَرَرَةٍ
“Sivyo katu! Hakika hizi ni Ukumbusho. Basi atakaye akumbuke. [Zimeandikwa] katika swahifa zilizokirimiwa. Zimetukuzwa na zimetwaharishwa. [Zinazobebwa] mikononi mwa waandishi, watukufu na watiifu.”[2]
Bi maana Malaika. Kama alivosema Mola wetu:
وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ الشَّيَاطِينُ وَمَا يَنبَغِي لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ إِنَّهُمْ عَنِ السَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ
”Na wala hawakuteremka nayo [Qur-aan hii] mashaytwaan na wala haipasi kwao na wala hawawezi. Hakika wao bila shaka wametengwa mbali kutokana na kuisikiliza.”[3]
[1] 56:79
[2] 80:11-16
[3] 26:210-212
- Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 83
- Imechapishwa: 20/03/2024
Swali: Je, inafaa kwa mwanamke mwenye hedhi na mwenye damu ya uzazi kugusa Qur-aan na kusoma ndani yake khaswa katika mwezi wa Ramadhaan wenye baraka ambao watu wanapupia kukhitimisha Qur-aan?
Jibu: Sijui kizuizi juu ya hilo. Hadiyth isemayo:
“Haigusi Qur-aan isipokuwa aliye msafi.”
Wako wanaosema kuwa kuna Swahabah anayekosekana katika cheni ya wapoezi. Tukikadiria kuwa ni nzuri kwa mkusanyiko wa njia zake inafasiriwa kama alivosema ash-Shawkaaniy katika “Nayl-ul-Awtwaar”:
“Haigusi Qur-aan isipokuwa aliye msafi.”
“Maana yake ni muislamu.”
Kwa maana nyingine haigusi ambaye ni kafiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza mtu kusafiri na Qur-aan kwenda katika miji ya maadui.
Kuhusu maneno Yake (Ta´ala):
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
“Hawaigusi isipokuwa waliotwahara.”[1]
Kinachokusudiwa ni Malaika. Hivo ndivo amesema Imaam Maalik katika “al-Muwattwa´”. Akaongezea kwamba Aayah hiyo inafasiriwa na maneno Yake (Ta´ala):
كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ بِأَيْدِي سَفَرَةٍ كِرَامٍ بَرَرَةٍ
“Sivyo katu! Hakika hizi ni Ukumbusho. Basi atakaye akumbuke. [Zimeandikwa] katika swahifa zilizokirimiwa. Zimetukuzwa na zimetwaharishwa. [Zinazobebwa] mikononi mwa waandishi, watukufu na watiifu.”[2]
Bi maana Malaika. Kama alivosema Mola wetu:
وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ الشَّيَاطِينُ وَمَا يَنبَغِي لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ إِنَّهُمْ عَنِ السَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ
”Na wala hawakuteremka nayo [Qur-aan hii] mashaytwaan na wala haipasi kwao na wala hawawezi. Hakika wao bila shaka wametengwa mbali kutokana na kuisikiliza.”[3]
[1] 56:79
[2] 80:11-16
[3] 26:210-212
Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 83
Imechapishwa: 20/03/2024
https://firqatunnajia.com/mwanamke-mwenye-hedhi-na-nifasi-anataka-kukhitimisha-qur-aan-ramadhaan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)