Swali: Ni ipi hukumu ya wanawake kutoka hali ya kujipamba na kujitia manukato kwa ajili ya kuswali Tarawiyh hali ya kuamini kwamba wanafanyia kazi maneno Yake Allaah (Ta´ala):
خُذُوا زِينَتَكُمْ عِندَ كُلِّ مَسْجِدٍ
“Chukueni mapambo yenu katika kila swalah.”[1]?
Jibu: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amewaruhusu wanawake kutoka kwenda kuswali ´Ishaa msikitini kwa sharti watoke hali ya kujisitiri vizuri, kwa maana ya kwamba wamevaa mavazi ambayo hayavutii kuelekezewa macho na pasi na kujitia manukato. Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwanamke yeyote anayetoka hali ya kujitia manukato ili wanuse harufu yake, basi ni mzinifu.”
[1] 07:31
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 86
- Imechapishwa: 21/03/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)