Swali: Je, kunawekwa sharti kule wanandoa kuendana na kulingana (الكفاءة) kwa upande wa nasabu zao?
Jibu: Hapana, sio sharti. Walingane kidini:
فَإِنْ عَلِمْتُمُوهُنَّ مُؤْمِنَاتٍ فَلَا تَرْجِعُوهُنَّ إِلَى الْكُفَّارِ ۖ لَا هُنَّ حِلٌّ لَّهُمْ وَلَا هُمْ يَحِلُّونَ لَهُنَّ
“Na mkiwatambua kuwa ni waumini basi msiwarejeshe [Makkah] kwa makafiri – wao si [wake]halali kwao [hao makafiri] na wala wao si [waume]halali kwao.” (60:10)
إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ
”Hakika aliye mbora zaidi miongoni mwenu mbele ya Allaah ni yule mwenye kumcha Allaah zaidi kati yenu.” (49:13)
Walingane na kuendana kidini. Muislamu asimuoe mwanamke wa kishirikina, kwa sababu Allaah anasema:
وَلَا تُنكِحُوا الْمُشْرِكِينَ حَتَّىٰ يُؤْمِنُوا
”Na wala msiwaoze wanaume washirikina mpaka waamini.” (02:221)
لَا هُنَّ حِلٌّ لَّهُمْ وَلَا هُمْ يَحِلُّونَ لَهُنَّ
“Wao [wanawake wa kiislamu] si halali kwao [hao makafiri] na wala wao [waume] si halali kwao.” (60:10)
Vivyo hivyo kuna uchambuzi kati ya muungwana na mtumwa.
Swali: Anayesema wa kijani?
Jibu: Hili ni jambo jipya kati ya watu wasiokuwa wasomi. Vinginevyo msingi ni mwarabu na asiyekuwa mwarabu. Huu ndio msingi. Baadhi wanalingana na wengine:
إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ
”Hakika aliye mbora zaidi miongoni mwenu mbele ya Allaah ni yule mwenye kumcha Allaah zaidi kati yenu.”
Swali: Baadhi wanajengea hoja maneno ya ´Umar aliyesema:
“Nitawazuia wale wanawake wenye nasabu wasiolewe isipokuwa na wale wanaolingana nao.”?
Jibu: Ikiwa imesihi[1], basi hiyo ni Ijtihaad yake.
[1] adh-Dhahabiy amesema:
”Ndani yake [kwenye cheni yake ya wapokezi yuko al-Haarith bin ´Imraan al-Ja´fariy ambaye anatuhumiwa uwongo na ´Ikrimah amemdhoofisha.” (Talkhiysw ´alaal-Mustadrak (02/02).
Ibn Qudaamah katika ”al-Mughniy” (09/388) amemnukuu Ibn ´Abdil-Barr ambaye amesema:
”Huyu ni mnyonge na hana msingi na wala hakujengewi hoja kwa mtu mfano wake.”
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23212/هل-تشترط-الكفاءة-بين-الزوجين-في-النسب
- Imechapishwa: 28/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)