Swali: Baadhi ya waume wanawakataza wake zao kufunga swawm zinazopendeza?

Jibu: Hapana vibaya kwao. Yeye mume anamuhitajia kustarehe naye. Kwa hiyo akimkataza basi ni sawa kufanya hivo.

Swali: Baadhi yao wanakuwa safarini?

Jibu: Hapana, akiwa msafiri basi hana haki ya kufanya hivo.

Swali: Anamwambia asifunge kwa sababu ya afya yake, uzuri wake na kadhalika.

Jibu: Hapana, hana haki. Akisafiri basi inafaa kwa mke kufunga kutokana na dalili ya Hadiyth.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/21969/حكم-منع-الزوج-زوجته-من-صيام-التطوع
  • Imechapishwa: 08/10/2022