Swali: Ni yupi bora aliyeandika kuhusu roho? Je, ni sahihi kuwa kitabu cha Imaam Ibn-ul-Qayyim (Rahimahu Allaah) “ar-Ruuh” alikiandika mwanzoni wakati alipokuwa Suufiy[1]?
Jibu: Ndio, wanasema hivi kwa lengo la kumpa udhuru. Kitabu kina faida kubwa na kuna mambo ambayo yanahitajiwa kuangaliwa. Hata hivyo ndani yake kuna faida na maudhui kubwa. Hivi kimehakikishwa na kuchapishwa vizuri. Mtu achukue faida nzuri zilizomo humo na aache mambo yenye kutatiza. Allaah ndiye Anajau zaidi alikiandika lini. Ni sahihi ya kwamba alikuwa Suufiy. Yeye mwenyewe alikubali hilo. Amekubali kosa lake wakati aliposema:
Ee watu wangu! Ninaapa kwa Allaah, Mtukufu
Hii ni nasaha ni nasaha ya ndugu yenu alo na wasiwasi na msaidizi
Nimejaribu yote haya
na nikatumbukia kwenye wavu nilipokuwa naruka
mpaka hapo Allaah Aliponitunukia
ambaye si mkono wala ulimi wangu hauwezi kumfidia
mwanachuoni kutoka Harraan
Allaah Amjaze kheri kweli kweli
kwa Pepo na radhi
Alinishika mkono na kwenda na mimi
mpaka akanionyesha inapotoka imani
Yeye mwenyewe amekubali hilo kwenye “an-Nuuniyyah”. Mwanzoni alikuwa na Taswawwuf na maoni yanayohitajiwa kuangaliwa. Wakati alipokutana na kigogo huyu Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah akanufaika naye, akajifunza haki na akapata elimu ya kubobea na ukaguzi. Allaah Amrahamu.
[1] Tazama al-Fawzaan kuhusu kitabu cha Ibn-ul-Qayyim “ar-Ruuh” – al-Firqah an-Naajiyah (firqatunnajia.com)
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy fiyl-´Aqiydah (07) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/qir-14340205.mp3
- Imechapishwa: 17/06/2015
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)