Swali: Mtoto wangu ana miaka 26. Haswali swalah za faradhi. Nimemnasihi mara nyingi, lakini pasi na mafanikio. Nifanye nini na yeye ili mimi mwenyewe nisiwe ni mwenye kutenda dhambi?

Jibu: Ikiwa anaweza kuishi kwa kujitegemea mtimue. Na ikiwa hawezi kuishi kwa kujitegemea kuwa na subira naye, mpe matumizi na endelea kumuamrisha kuswali. Allaah atakusaidia na kumwongoza na kuufungua moyo wake – Allaah akitaka. Usikate tamaa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy fiyl-´Aqiydah (07) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/qir-14340205.mp3
  • Imechapishwa: 17/06/2015