Swali: Msemo unaosema:
“Hakuna hayaa katika dini.”
ni sahihi?
Jibu: Sijui msingi wake. Msemo huo umechukuliwa kutoka katika maneno ya Umm Sulaym alisema maneno yenye maana kama:
“Ee Mtume wa Allaah! Hakika Allaah hastahi juu ya haki.”
Msemo huo umechukuliwa kutoka hapa. Akauliza:
“Ee Mtume wa Allaah! Je, ni lazima kwa mwanamke kuoga josho ya janaba anapoota?”
Akauliza na kwamba si mwenye kuona hayaa kwa sababu anauliza jambo muhimu. Akamjibu:
“Ndio. Akiona manii.”
Isitoshe Allaah (Ta´ala) amesema:
وَاللَّهُ لَا يَسْتَحْيِي مِنَ الْحَقِّ
“ Allaah hastahi haki.”[1]
[1] 33:53
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22688/ما-صحة-قول-لا-حياء-في-الدين
- Imechapishwa: 18/07/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)