Swali: Baadhi ya wasafiri wanaingia misikitini na wanakuta kuna Jamaa´ah inayotaka kusimamishwa. Wanasubiri mpaka imamu aswali Rak´ah mbili ikiwa ni swalah ya Rak´ah nne kisha wanajiunga naye katika Rak´ah mbili za mwisho kwa hoja ya kwamba wao ni wasafiri wanafupisha.
Jibu: Hili si sawa, haijuzu na swalah zao hazisihi. Wanachotakiwa ni kuingia pamoja na imamu na kuswali kikamilifu swalah zao. Kwa kuwa hukumu zao ni hukumu za Imamu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Imamu amewekwa ili afuatwe.”
Msafiri akiswali nyuma ya mkazi anachotakiwa ni kuswali kikamilifu swalah zake. Lakini kusubiri mpaka kunapobaki Rak´ah mbili, ni nani aliewatolea fatwa hii? Huu ni ujinga na haijuzu. Swalah zao hazisihi kwa kuwa hukumu yao ni hukumu ya Imamu. Imamu anaswali kikamilifu hivyo na wao wanalazimika kuswali kikamilifu.
Hata kama hawakuwahi pamoja na Imamu isipokuwa Tashahhud ya mwisho, wanalazimika kuswali kikamilifu. Kwa kuwa hukumu yao ni hukumu ya Imamu.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/liqo-01-08-1435-01.mp3
- Imechapishwa: 03/05/2015
Swali: Baadhi ya wasafiri wanaingia misikitini na wanakuta kuna Jamaa´ah inayotaka kusimamishwa. Wanasubiri mpaka imamu aswali Rak´ah mbili ikiwa ni swalah ya Rak´ah nne kisha wanajiunga naye katika Rak´ah mbili za mwisho kwa hoja ya kwamba wao ni wasafiri wanafupisha.
Jibu: Hili si sawa, haijuzu na swalah zao hazisihi. Wanachotakiwa ni kuingia pamoja na imamu na kuswali kikamilifu swalah zao. Kwa kuwa hukumu zao ni hukumu za Imamu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Imamu amewekwa ili afuatwe.”
Msafiri akiswali nyuma ya mkazi anachotakiwa ni kuswali kikamilifu swalah zake. Lakini kusubiri mpaka kunapobaki Rak´ah mbili, ni nani aliewatolea fatwa hii? Huu ni ujinga na haijuzu. Swalah zao hazisihi kwa kuwa hukumu yao ni hukumu ya Imamu. Imamu anaswali kikamilifu hivyo na wao wanalazimika kuswali kikamilifu.
Hata kama hawakuwahi pamoja na Imamu isipokuwa Tashahhud ya mwisho, wanalazimika kuswali kikamilifu. Kwa kuwa hukumu yao ni hukumu ya Imamu.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/liqo-01-08-1435-01.mp3
Imechapishwa: 03/05/2015
https://firqatunnajia.com/msafiri-kusubiri-na-kujiunga-na-imamu-katika-rakah-mbili-za-mwisho/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)