Swali: Imethibiti kwa Mitume (Swalla Allaahu ´alayhim wa sallam) kumuona Allaah usingizini?
Jibu: Shaykh Taqiyy-ud-Diyn Ibn Taymiyyah ametaja kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaweza kuona nuru au maneno. Allaah hafanani na viumbe Wake (Subhaanahu wa Ta´ala).
Swali: Vipi kuhusu Muusa na ´Iysaa (Swalla Allaahu ´alayhimaa wa sallam)?
Jibu: Allaah ndiye mjuzi zaidi. Hatujafikiwa na kitu.
Swali: Kumuona Allaah inahesabika ni kitu maalum kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?
Jibu: Hapana. Hata Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakumuona. Alipoulizwa alisema:
”Niliona nuru. Ni vipi nitamuona?”
Vilevile Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Tambueni kuwa hakuna yeyote katika nyinyi atamuona Mola wake mpaka afe.”
Kumuona Allaah kunakuwa Aakhirah. Waumini watamuona siku ya Qiyaamah na watamuona Peponi. Kuhusu duniani hapana.
Swali: Vipi kuhusu kumuona usingizini?
Jibu: Kuhusu kumuona usingizini kunaweza kutokea.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22261/هل-تثبت-روية-الله-تعالى-في-المنام-للانبياء
- Imechapishwa: 27/01/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)