Swali: Kuanza kutoa salamu ni lazima au inapendeza?
Jibu: Allaah ndiye anajua zaidi. Hata hivyo udhahiri wa Hadiyth ni kwamba inapaswa kwa muumini asifanye uchoyo. Aharakishe kutoa salamu. Hii ndio Sunnah kwa muumini. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Haki ya muislamu juu ya muislamu mwenzie ni sita; ukikutana naye mtoe salamu.”
al-Baraa´ amesema:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameamtuamrisha mambo saba” ambapo akataja moja wapo kueneza salamu.”
Kwa hivyo inatakikana kwa mtu kuiharakisha. Ni mamoja tuseme kuwa inapendeza kufanya hivo au ni lazima. Kuhusu kujibu ni lazima.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ttps://binbaz.org.sa/fatwas/22274/هل-البدء-بالسلام-للوجوب-ام-للاستحباب
- Imechapishwa: 27/01/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)