Swali: Imeenea katika njia za mawasiliano mtu ambaye amemuota Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na amempa wasia na akamuahidi furaha endapo ataeneza wasia huu na huzuni na majuto endapo hatofanya hivo.
Jibu: Ni shaytwaan. Sio kila anayemuota Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amemuona kweli. Yule mtu ambaye anazijua sifa za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndiye ambaye anaweza kumuona. Shaytwaan hawezi kujifananisha na umbile lake ya kihakika. Mtu ambaye hazijui sifa za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) asiaminiwe. Kuna uwezekano ikawa ni shaytwaan.
Jengine ni kwamba wasia na maamrisho yamekatika kwa kufa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hakuna maamrisho, wasia wala na mambo ya Shari´ah baada ya kufa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Yale ambayo Allaah ametuwekea katika Shari´ah yanatosheleza. Shari´ah ya Kiislamu inatutosheleza. Hatutaki kuwa na ziada, maamrisho, mahamasisho ya kueneza na kadhalika.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Tafsiyr-ish-Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (25) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ayatquran-26-07-1435-01.mp3
- Imechapishwa: 20/06/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)