Swali: Ni ipi hukumu ya kupiga makofi?
Jibu: Kupiga makofi ni katika matendo kabla ya kuja kwa Uislamu. Haitakikani. Ikihitajika basi watu walete Takbiyr kama inavofanywa ndani ya swalah ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kupiga makofi ni kwa wanawake na Tasbiyh ni kwa wanaume.”
Isitoshe Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَمَا كَانَ صَلَاتُهُمْ عِندَ الْبَيْتِ إِلَّا مُكَاءً وَتَصْدِيَةً
“Na haikuwa swalaah zao katika Nyumba isipokuwa ni miluzi na kupiga makofi.”[1]
Wanazuoni wamesema kuwa (المكاء) ni kupiga miluzi na (التصدية) ni kupiga makofi.
Swali: Kwa hiyo ni haramu?
Jibu: Dogo liwezelo kusemwa ni kwamba inachukiza. Kuna uwezekano mkubwa ikawa ni haramu. Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kupiga makofi ni kwa wanawake… “
kunafahamisha kuwa sio katika matendo ya wanaume. Ni katika matendo ya wanawake au makafiri.
[1] 08:35
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23091/ما-حكم-التصفيق
- Imechapishwa: 28/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)