Swali: Ni ipi alama za usiku wa Qadr? Ni kipi kinachompasa muislamu katika usiku huo?
Jibu: Inapendeza kusimama usiku wa Qadr. Ni usiku umewekwa maalum katika yale masiku kumi ya mwisho ya Ramadhaan. Zile nyusiku za witiri zina uhakika zaidi kuliko nyenginezo. Kilichowekwa katika Shari´ah ni kujitahidi kumtii Allaah (Jalla wa ´Alaa) katika michana na nyusiku hizi kumi. Kusimama usiku kuswali si jambo la lazima. Ni kitu kinapendeza. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akijitahidi katika masiku kumi ya mwisho kuliko anavofanya katika masiku mengine. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ilikuwa zinapoingia zile siku kumi za mwisho basi anahuisha usiku, anaiamsha familia yake, anakuwa jadi na hufunga vizuri kikoi chake.”[1]
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule atakayesimama kuswali usiku wa Qadr kwa imani na kwa matarajio, basi atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.”[2]
Kuna Hadiyth nyingi zenye maana kama hiyo.
[1] al-Bukhaariy (1884) na Muslim (2008).
[2] al-Bukhaariy (1768) na Muslim (1268).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (15/431)
- Imechapishwa: 15/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)