Swali: Je, inafaa nikaswali Witr mbili katika usiku mmoja?
Jibu: Haitakikani kwa yeyote kuswali Witr mbili katika usiku mmoja. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakuna Witr mbili katika usiku mmoja.”[1]
“Ifanye swalah yenu ya mwisho usiku ni Witr.”[2]
“Anayechelea kutoamka mwisho mwa usiku basi aamche mwanzoni mwake, na anayetaraji kuamka mwishoni mwake basi aswali Witr mwishoni mwa usiku. Hakika swalah mwishoni mwa usiku ni yenye kushuhudiwa – na hilo ndio bora.”[3]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Ikiwezekana kwa muislamu kuiswali Tahajjud yake mwishoni mwa usiku, basi aimalize swalah yake kwa Rak´ah moja awitirishe kwayo. Na asiyeweza hilo basi aswali Witr mwanzoni mwa usiku. Allaah akimfanyia wepesi kuamka kuswali kisimamo cha usiku mwishoni mwa usiku, basi ataswali shafwa awezavyo Rak´ah mbilimbili na asirudi kuleta Witr. Ile Witr yake ya kwanza inatosha kutokana na Hadiyth iliotangulia pale ambapo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliposema:
“Hakuna Witr mbili katika usiku mmoja.”
[1] at-Tirmidhiy (432) na an-Nasaa´iy (1661).
[2] al-Bukhaariy (943) na Muslim (1245).
[3] Muslim (1255).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/310)
- Imechapishwa: 04/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)