Swali: Makatazo ya kuharakia swalah na kulazimiana na utulivu na upole.
Jibu: Kinachotambulika kwa wanazuoni ni kwamba haya ni makatazo ya machukizo. Muumini anatakiwa kujipamba kwa adabu alizobainisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Swali: Wako ambao wamefunganisha makatazo ya kukimbia wakati kunapokimiwa swalah na kwamba asifanye haraka kwa hali zote au jambo hilo ni pale tu kunapokimiwa swalah tu?
Jibu: Asifanye haraka kabisa; si wakati kunapokimiwa wala nyakati zingine. Atembee kwa utulivu.
Swali: Je, jambo hilo sio maalum kwa ajili ya ijumaa?
Jibu: Hakuna umaalum wa chochote.
Swali: Vipi mtu kufanya haraka kwa ajili ya kuwahi Rak´ah ya mwisho?
Jibu: Haijalishi kitu. Akiikosa ataikidhi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23711/حكم-الاسراع-في-المشي-الى-الصلاة
- Imechapishwa: 12/04/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)