23. Kitabu kilichoko kwa Allaah juu ya ´Arshi

21 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Wakati Allaah (´Azza wa Jall) alipohukumu viumbe aliandika katika kitabu Chake kilichoko Kwake juu ya ´Arshi: ”Hakika huruma Yangu inashinda ghadhabu Zangu.”[1]

Imekuja Katika tamko jengine:

“Allaah kabla hajaumba viumbe aliandika kitabu: “Hakika huruma Yangu inashinda ghadhabu Zangu.” Kiko Kwake juu ya ´Arshi.”

Imekuja Katika tamko jengine:

”Wakati Allaah alipoumba viumbe, aliandika kitabu juu yake Mwenyewe. Kimenyanyuliwa juu ya ´Arshi: “Hakika huruma Yangu inashinda ghadhabu Zangu.”[2]

[1] al-Bukhaariy (3194), Muslim (2751), Ahmad (2/466) na wengineo.

[2] Hadiyth ni Swahiyh. Baadhi ya matamshi yake yapo kwa al-Bukhaariy na Muslim. Tamko la mwisho liko kwa at-Tirmidhiy. Nimeitaja katika “as-Swahiyhah” (1629) na ”Dhwilaal-ul-Jannah fiy Takhriyj-is-Sunnah” (810-811).

  • Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk 92
  • Imechapishwa: 12/04/2024
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy