Swali: Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Watu walipita na jeneza na wakalisifu ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Imewajibika.” Kisha kukapita jeneza lingine ambalo wakalisema vibaya. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Imewajibika.” Ndipo ´Umar akasema: “Ee Mtume wa Allaah! “Watu wamepita na jeneza na wakalisifu ambapo ukasema: “Imewajibika.” na wakapita na jeneza lingine ambalo wakalisema vibaya na wewe ukasema: “Imewajibika.” ndipo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Nyinyi ni mashahidi wa Allaah juu ya ardhi. Nyinyi ni mashahidi wa Allaah juu ya ardhi. Nyinyi ni mashahidi wa Allaah juu ya ardhi.”[1]
Jibu: Maana yake ni sahihi. Maana yake ni kwamba mtu anayedhihirisha maovu na shari basi hapana vibaya kumsengenya. Ndio maana akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Imewajibika.”
Bi maana Moto umemuwajibikia. Huyu ni yule ambaye alikuwa akifanya maovu hadharani na watu wakimweleza kuwa na kheri na kadhalika. Ndipo akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Imewajibika.”
Hapana vibaya kumsengenya. Ni yule anayedhihirisha madhambi.
[1] Ameipokea al-Bukhaariy (1367) na Muslim (949).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23121/معنى-حديث-مروا-بجنازة-فاثنوا-عليها-شرا
- Imechapishwa: 04/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)