Swali: Dada huyu anauliza hukumu ya Qur-aan inayoandikwa na kutundikwa nyumbani au kuvaliwa ikawa kama ni Hijaab?
Jibu: Hili halijuzu. Haijuzu kutundika Qur-aan kwa njia ya Hijaab. Hili limekatazwa na Salaf. Kauli sahihi ya wanachuoni ni kwamba haijuzu. Hata kama ni Qur-aan mtu asiitundike. Hata hivyo anaweza kusomewa Qur-aan. Hili ni jambo zuri. Ama kuhusu kuitundika haijuzu hata kama itakuwa ni Qur-aan.
Ama ikiwa [kilichoandikwa] ni kitu kingine mbali na Qur-aan, kama ushirikina na mambo ya uchawi, hili kwa makubaliano ni kwamba haijuzu. Ni hirizi za kishirikina. Vinavyotundikwa au kuvaliwa vimegawanyika aina mbili:
1- Qur-aan. Hili lina tofauti. Kauli sahihi ni kuwa haijuzu.
2- Mambo ya ushirikina na ya uchawi na matamshi ya kiajabu yasiyofahamika. Hili ni haramu kwa makubaliano. Ni Shirki.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kitaab Ahaadiyth-il-Fitnah http://www.alfawzan.af.org.sa/node/15243
- Imechapishwa: 21/04/2015
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket