Swali: Je, imewekwa katika Shari´ah kwa taasisi ya Kiislamu ya kimataifa kuchukua Zakaat-ul-Fitwr mwanzoni mwa Ramadhaan ili kuweza kufaidika nayo kwa kiasi kinachowezekana?
Jibu: Sionelei kufaa kufanya hivo. Wala sionelei kufaa kutoa Zakaat-ul-Fitwr nje ya nchi anayoishi mtu. Watu wanaoshi katika nchi hiyo wana haki zaidi ya Zakaat-ul-Fitwr hiyo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema kumwambia Mu´aadh bin Jabal wakati alipomtuma Yemen:
”Wafunze kwamba Allaah amefaradhisha juu ya mali yao zakaah itayochukuliwa kutoka kwa matajiri wao na kupewa mafukara wao.”
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (18/268)
- Imechapishwa: 04/05/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket