Swali: Je, wanapata thawabu kutokana maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Simameni hali ya kuwa mmesamehewa kutoka katika vikao vyenu vya kumtaja Allaah?”
Jibu: Hapana shaka. Wanashukiwa na utulivu, wanafunikwa na rehema, wanazungukwa na Malaika na Allaah anawataja kwa wale walioko Kwake. Hizi ni fadhilah kuu. Rehema inawazunguka na Allaah anawataja kwa wale walioko Kwake. Allaah atujaalie sisi na nyinyi kuwa miongoni mwao. Hii ni fadhilah Yake (´Azza wa Jall). Lakini muhimu ni mtu kumtakasia nia Allaah juu ya hilo, kuwa mkweli na kutojionyesha.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23093/معنى-قوموا-مغفورا-لكم-لمجالس-الذكر
- Imechapishwa: 28/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)