Swali: Je, swalah ya usiku na kisomo ndani yake inakuwa kimyakimya au kwa sauti ya juu?
Jibu: Swalah ya usiku ni kwa sauti ya juu. Hata hivyo hapana neno akisoma kimyakimya. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisoma kimyakimya na alisoma kwa sauti ya juu. Akiona manufaa ni katika kusoma kimyakimya atafanya hivo, na akiona manufaa ni katika kusoma kwa sauti ya juu atafanya hivo. Ijapo kusoma kwa sauti ya juu ndio bora zaidi ikiwezekana. Na ikiwa kusoma kimyakimya ndio moyo wake unaingiwa na unyenyekevu zaidi basi hapana vibaya.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/9812/حكم-الجهر-والاسرار-في-صلاة-الليل
- Imechapishwa: 05/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)