Swali: Wakati Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa anaingia mahali walipo Maswahabah zake nao wamekaa alikuwa akiwasalimia kwa kupeana nao mkono au anawatolea salamu kisha anakaa pale kinapoishia kikao?
Jibu: Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiketi pale kinapoishilia kikao.
Swali: Akipeana nao mkono?
Jibu: Hatujafikiwa na hilo. Maswahabah walikuwa wanapeana mkono pindi wanapokutana na anapoingia basi hawasimami kwa ajili yake. Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaketi pale kinapoishia kikao.
Swali: Hadiyth inayozungumzia kupeana mkono?
Jibu: Ni Sunnah. Wakipeana mkono ni Sunnah. Lakini hatukufikiwa na khabari kuwa walikuwa wakisimama kwa ajili yake na kupeana mkono. Kwa sababu kitendo hicho kinaweza kuwakalifisha watu sana.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22240/حكم-المصافحة-لمن-دخل-على-قوم-جلوس
- Imechapishwa: 19/01/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)