Kuondoka punde tu baada ya kumalizika swalah ya mkusanyiko

Swali: Vipi kuhusu [mswaliji] kuondoka kabla ya kugeuka kwa imamu?

Jibu: Hapana vibaya. Akitoa salamu swalah imemalizika. Lakini bora aketi chini hadi amalize kusema:

أستغفر الله

“Allaah nisamehe.”

Mara tatu.

واللهم أنت السلام ومنك السلام تباركت يا ذا الجلال والإكرام

“Ee Allaah! Wewe ndiye as-Salaam, amani inatoka Kwako, umebarikika, Ee Mwenye utukufu na ukarimu.”

Baada ya hapo asome zile Adhkaar zilizowekwa katika Shari´ah. Hivi ndio bora. Vinginevyo akitoa salamu swalah imemalizika.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23039/حكم-انصراف-الماموم-قبل-ان-ينصرف-الامام
  • Imechapishwa: 20/10/2023