Swali: Lau muislamu atapeana mikono na myahudi au mnaswara wakati yuko na wudhuu´. Ana nini juu yake?
Jibu: Haifai kwake kupeana mikono na kafiri. Asimpe mkono. Akitoa salamu aseme: “wa ´alaykum.” Anasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Ahl-ul-Kitaab wakiwatolea salamu, semeni: “wa ´alaykum”.”
Asianze kumsalimia yeye na wala asimpe mkono. Lakini ikiwa yeye ataanza kukupa mkono na kukusalimia, wudhuu´ wake hauvunjiki. Wudhuu´ wake ni sahihi. Kumgusa kafiri hakutengui wudhuu´.
- Muhusika: Imaaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://subulsalam.com/catplay.php?catsmktba=155
- Imechapishwa: 19/11/2014
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)