Kutoka kwa Muhammad bin Ibraahiym kwenda kwa muheshimiwa X.
السلام عليكم ورحمة الله وبركاته
Tumefikiwa na barua unayosema kuwa uko na bibi ambaye amefikisha takriban miaka 50 na kwamba alifanyiwa upasuaji mwaka wa 1386 na kwamba daktari amemkataza kufunga na kwamba hivi sasa anaelekea kupona. Anasumbuliwa na maradhi ya kisukari na hawezi kulipa swawm anazodaiwa kwa kufululiza kwa sababu anatumia dawa ya kisukari mara tatu kwa siku na mengine uliyotaja. Unauliza kama inafaa kwake kufunga kwa kuachanisha siku?
Jawabu ni kwamba hapana vibaya kulipa swawm kwa kuachanisha siku. Lakini kwa sharti kwamba asifikiwe na Ramadhaan nyingine isipokuwa awe amemaliza deni la funga yake. Jengine ni kwamba swawm, kama walivosema madaktari wenyewe, ni miongoni mwa sababu za kupunguza kiwango cha sukari.
Muftiy wa Saudi Arabia
15/06/1387
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Ibraahiym Aalush-Shaykh
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (04/199-200)
- Imechapishwa: 19/03/2024
Kutoka kwa Muhammad bin Ibraahiym kwenda kwa muheshimiwa X.
السلام عليكم ورحمة الله وبركاته
Tumefikiwa na barua unayosema kuwa uko na bibi ambaye amefikisha takriban miaka 50 na kwamba alifanyiwa upasuaji mwaka wa 1386 na kwamba daktari amemkataza kufunga na kwamba hivi sasa anaelekea kupona. Anasumbuliwa na maradhi ya kisukari na hawezi kulipa swawm anazodaiwa kwa kufululiza kwa sababu anatumia dawa ya kisukari mara tatu kwa siku na mengine uliyotaja. Unauliza kama inafaa kwake kufunga kwa kuachanisha siku?
Jawabu ni kwamba hapana vibaya kulipa swawm kwa kuachanisha siku. Lakini kwa sharti kwamba asifikiwe na Ramadhaan nyingine isipokuwa awe amemaliza deni la funga yake. Jengine ni kwamba swawm, kama walivosema madaktari wenyewe, ni miongoni mwa sababu za kupunguza kiwango cha sukari.
Muftiy wa Saudi Arabia
15/06/1387
Mhusika: Imaam Muhammad bin Ibraahiym Aalush-Shaykh
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (04/199-200)
Imechapishwa: 19/03/2024
https://firqatunnajia.com/kulipa-deni-la-ramadhaan-kwa-kuachanisha-siku/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)