Swali: Inajuzu kukojoa kwa kusimama na kujipangusa kwenye kuta ikiwa kuna maji?
Jibu: Ndio. Yote mawili yanajuzu. Inajuzu kukojoa kwa kusimama, lakini lililo bora zaidi ni kukojoa kwa kukaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifanya yote mawili. Alikojoa kwa kukaa, jambo ambalo alikuwa akifanya mara nyingi, na alikojoa kwa kusimama. Inasemekena ni kwa kuwa alikuwa mgonjwa na imesemekana kuwa alifanya hivo kwa sababu ya kuonesha kuwa inajuzu. Maoni haya ya pili ndio sahihi. Lakini hata hivyo anatakiwa kujilinda na cheche za mkojo zisimrukie.
Inapokuja katika kujipangusa, anaweza kujipangusa kwa kuta, mawe au kitu kingine chenye kuchukua nafasi ya mawe midhali kitu hicho kinasafisha na kukausha. Haina neno.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (02) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/omdh–14340204.mp3
- Imechapishwa: 25/08/2020
Swali: Inajuzu kukojoa kwa kusimama na kujipangusa kwenye kuta ikiwa kuna maji?
Jibu: Ndio. Yote mawili yanajuzu. Inajuzu kukojoa kwa kusimama, lakini lililo bora zaidi ni kukojoa kwa kukaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifanya yote mawili. Alikojoa kwa kukaa, jambo ambalo alikuwa akifanya mara nyingi, na alikojoa kwa kusimama. Inasemekena ni kwa kuwa alikuwa mgonjwa na imesemekana kuwa alifanya hivo kwa sababu ya kuonesha kuwa inajuzu. Maoni haya ya pili ndio sahihi. Lakini hata hivyo anatakiwa kujilinda na cheche za mkojo zisimrukie.
Inapokuja katika kujipangusa, anaweza kujipangusa kwa kuta, mawe au kitu kingine chenye kuchukua nafasi ya mawe midhali kitu hicho kinasafisha na kukausha. Haina neno.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (02) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/omdh–14340204.mp3
Imechapishwa: 25/08/2020
https://firqatunnajia.com/kukojoa-kwa-kusimama-na-kujipangusa-na-kuta/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)