Swali: Baadhi ya watu wanapotaka kunywa na mkononi mwake kukawa kuna mafuta basi anaweka mkono wake chini ya kikombe.
Jibu: Hapana vibaya kujisaidia kwa mkono wa kushoto. Ajisaidie kwa mkono wa kushoto haja ikimpelekea kufanya hivo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akijisaidia nao wakati wa kuvunja mfupa, anachukua kisu na anajisaidia kwa mkono wa kushoto. Ni sawa haja ikipelekea kujisaidia kwa mkono wa kushoto.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/21937/حكم-الاستعانة-باليد-اليسرى-في-الاكل-والشرب
- Imechapishwa: 12/01/2023