Swali: Je, inafaa kwa mtu ambaye ametia shaka kuanza kwa Ramadhaan kufunga siku moja kabla yake?
Jibu: Wako katika Hanaabilah wenye kuonelea hivo. Lakini sahihi ni kwamba asifunge. Imethibiti kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Msiitangulizie Ramadhaan kwa kufunga siku moja au mbili.”[1]
´Ammaar (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia:
“Yeyote mwenye kufunga siku ya shaka, basi hakika amemuasi Abul-Qaasim.”[2]
Kwa hivyo maoni sahihi ni kwamba mtu asifunge. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Fungeni kwa kuuona na mfungue kwa kuuona. Mkifunikwa na mawingu, basi kamilisheni idadi ya Sha´baan thelathini.”[3]
Kwa hivyo hakuna kilichobaki baada ya ubainifu huu.
[1] al-Bukhaariy (1914) na Muslim (1082).
[2] al-Bukhaariy (03/27).
[3] al-Bukhaariy (1909).
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 75
- Imechapishwa: 15/03/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)