Swali: Ni ipi hukumu ya mtu anayechinja wanyama kwenye kaburi la maiti baada ya kuzikwa kwa nia ya swadaqah kwa roho yake?

Jibu: Hili ni maovu. Haijuzu. Zamani kabla ya kuja Uislamu walikuwa wakiliita “´Aqr”; walikuwa wakikaa karibu na kaburi lake na wakipita walichinja hapo kwa ajili yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Hakuna ´Aqr katika Uislamu.”

Vivyo hivyo wakichinja kwenye kaburi lake kwa kusudio la swadaqah, hili halijuzu. Hii ni Bid´ah. Ni maovu.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/3519/حكم-الذبح-عند-قبر-الميت-بعد-دفنه-صدقة-عليه
  • Imechapishwa: 05/09/2026