Hukumu ya aliyesahau kutaja jina la Allaah kabla ya wudhuu´

Swali: Ni ipi hukumu ya mtu aliyesahau kutaja jina la Allaah kabla ya kutawadha?

Jibu: Kumedondoka kutoka kwake kutaja jina la Allaah mwanzoni mwa wudhuu´. Hivyo akilisahau, basi hakuna kitu juu yake. Akiikumbuka katikati ya wudhuu´, basi atasema wakati huo, atasema:

بسم الله

”Naanza kwa jina la Allaah.”

Ni kama ilivyo katika kula; anataja jina la Allaah wakati wa kula. Akiisahau mwanzoni, hulitaja katikati.

Kuhusu Hadiyth ni dhaifu. Lakini lililo wajibu ni kwamba akiikumbuka ataje. Hili ndilo linalofaa ili kutoka katika makinzano ya wanazuoni. Wanazuoni wengi wanaona kuwa ni Sunnah, kwa sababu Hadiyth ni dhaifu. Lakini akiiacha kwa makusudi, inafaa arudie wudhuu´. Ama ikiwa ni kwa ujinga au kwa kusahau, hakuna ubaya.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/3521/حكم-من-نسي-التسمية-قبل-الوضوء
  • Imechapishwa: 05/09/2026