Swali: Unasemaje juu ya maneno ya Imaam Ahmad:
”Mwenye kuacha Witr kwa kuendelea ni mtu fasiki”?
Jibu: Alisema kuwa ni mtu muovu. Hii ni Ijtihaad yake. Witr sio lazima. Bali ni Sunnah inayokokoteza na sio lazima. Hata hivyo maneno yake si sahihi kwa upande wa dalili za Kishari´ah.
Swali: Mtu akiiacha anakuwa mwenye kutenda dhambi?
Jibu: Hapana, si mwenye kupata dhambi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati alipomfunza bwana mmoja swalah tano bwana huyo alimuuliza:
”Je, kuna nyenginezo zinazonilazimu, ee Mtume wa Allaah?” Akamwambia: ”Hapana, isipokuwa ukijitolea.””
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/21926/حكم-الخلوة-بالمحرم-الذي-لا-يخاف-الله
- Imechapishwa: 12/01/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)