Allaah (´Azza wa Jall) Amesema:

وَمِنَ النَّاسِ مَن يُعْجِبُكَ قَوْلُهُ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَيُشْهِدُ اللَّـهَ عَلَىٰ مَا فِي قَلْبِهِ وَهُوَ أَلَدُّ الْخِصَامِ وَإِذَا تَوَلَّىٰ سَعَىٰ فِي الْأَرْضِ لِيُفْسِدَ فِيهَا وَيُهْلِكَ الْحَرْثَ وَالنَّسْلَ ۗ وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ الْفَسَادَ وَإِذَا قِيلَ لَهُ اتَّقِ اللَّـهَ أَخَذَتْهُ الْعِزَّةُ بِالْإِثْمِ ۚ فَحَسْبُهُ جَهَنَّمُ ۚ وَلَبِئْسَ الْمِهَادُ

”Katika watu yuko anayekuvutia kauli yake katika uhai wa dunia na humshuhudisha Allaah kwa yale yaliyomo ndani ya moyo wake na hali yeye ndiye mpinzani muovu zaidi. Na anapoondoka hufanya bidii katika ardhi ili afisidi humo na aangamize mimea na vizazi; Allaah hapendi uharibifu. Anapoambiwa ´Mche Allaah!`, basi hupandwa kiburi kinachompeleka kutenda madhambi. Basi Jahannam inamtosheleza – na mahali pabaya palioje pa kupumzikia!” (02:204-206)

Allaah ni Mkubwa! Ni uzuri ulioje Aayah zinavyowagusa Khawaarij wa leo ambao wanaeneza ufisadi katika ardhi? Wanafungua njia ya hujuma na [wana] njaa kwa ajili hilo. Wanasema kuwa ni Jihaad. Uhakika wa mambo ni kwamba ni katika ufisadi mkubwa, umwagaji wa damu, machafuko, uharibifu wa mali na kuenea khofu kwa watu wasio na hatia. Huu ni ugaidi.

Hakuna shaka yoyote kwamba mimi na wengine tunaonelea kuwa watu hawa watapata mwisho mbaya kwa Allaah na matumaini yao juu ya uokovu yako mbali kabisa. Kwa sababu wameenda kinyume na maandiko ya Shari´ah na nasaha za wenye busara.

  • Muhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ar-Radd al-Muhabbar, uk. 56-57
  • Imechapishwa: 23/04/2015