Swali: Mwenye kukaa I´tikaaf anaianza kuanzia Fajr ya tarehe ishirini au usiku wa tarehe ishirini?
Jibu: Aanze I´tikaaf Fajr ya tarehe ishirini na moja. Hapana vibaya akilala usiku huo hali ya kuwa ni mwenye kukaa I´tikaaf. Lakini ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiingia I´tikaaf yake akishaswali Fajr.”
Bi maana kuanzia tarehe ishirini na moja.
Swali: Je, usiku wa Qadar si unakuwa usiku wa tarehe ishirini na moja?
Jibu: Ndio, unaweza kuwa tarehe 21 na 23. Unahamahama katika nyusiku zote kumi za Ramadhaan. Iliwahi kutokea usiku wa Qadar ukaangukia tarehe ishirini na moja katika zama za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Swali: Kwa hiyo mwenye kukaa I´tikaaf anaingia baada ya Fajr?
Jibu: Ataswali pamoja na waislamu msikitini hata kama hajaanza kukaa I´tikaaf.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22333/متى-يبدا-وقت-الاعتكاف-في-رمضان
- Imechapishwa: 10/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)