Swali: Hadiyth inayosema fasiki hana usengenyi.
Jibu: Sitambui msingi wake. Hata hivyo ni yenye kuchukuliwa kutoka katika Hadiyth ambazo ni Swahiyh. Alipojiwa na bwana mmoja akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mwache aingie. Ndugu mbaya aliyoje!”[1]
Ikafahamisha kuwa hapana ubaya kumsengenya ambaye anadhihirisha uovu. Hadiyth iliyotangulia punde mmekwishaisikia ambapo lilipitishwa jeneza la mtu ambapo Maswahabah wakamsema vibaya akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Imewajibika.”[2]
Kwa hivyo mtu akidhihirisha shari na akafanya maasi hadharani basi inafaa kumsengenya katika yale aliyodhihirisha. Tunamuomba Allaah usalama.
Swali: Mtu anaweza kumsema…
Jibu: Hata baada ya kufa kwake kunapokuwa na haja ya kufanya hivo. Kwa lengo watu wasidanganyike naye.
[1] Ahmad (6/38), al-Bukhaariy (6032) na Muslim (2591).
[2] Ameipokea al-Bukhaariy (1367) na Muslim (949).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23200/ما-صحة-حديث-لا-غيبة-لفاسق
- Imechapishwa: 25/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)