Swali: Imamu kusubiri swalah?
Jibu: Anatakiwa kuchunga wakati unaofaa ili asiwatie watu uzito.
Swali: Nakusudia kwamba fadhilah za yeye kutangulia?
Jibu: Akitangulia msikitini hapana vibaya. Mtume (Swalla Allaahu ´´alayhi wa sallam) alikuwa akitoka wakati wa swalah. Lakini akiona kuwa manufaa ni yeye kutangulia msikitini hapana vibaya. Sijui kikwazo chochote.
Swali: Lakini kwa ajili ya kutafuta fadhilah hizi?
Jibu: Hapana neno. Kunatarajiwa kwake kheri.
Swali: Je, imesihi kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akija kabla ya kukimiwa?
Jibu: Sijafikiwa na chochote kuhusu hilo. Hata hivyo hapana vibaya. Hadiyth zinafahamisha ya kwamba ambaye atakuja mapema yuko na kheri kubwa.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23727/هل-يشرع-للامام-انتظار-الصلاة-بالمسجد
- Imechapishwa: 13/04/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)