Swali: Vipi ikiwa mtu atasujudu juu ya nguo yake?
Jibu: Haidhuru, hapana vibaya ikiwa atasujudu juu ya nguo yake.
Swali: Je, ikiwa atasujudu juu ya miiba?
Jibu: Ikiwa haiumizi, hakuna tatizo. Watu wengine wana ngozi ya paji la uso yenye ukakamavu na ikiwa haiumizi, basi hapana vibaya.
Swali: Je, inafaa kwake kuinua kichwa chake, kuondoa kitu hicho kisha arudi kwenye Sujuud?
Jibu: Ndio, ainue kichwa chake, aondoshe kile chenye kumkera, kisha aweke tena paji la uso wake chini.
Swali: Je, kusujudu juu ya mto?
Jibu: Bora zaidi kusujudu bila kitu. Ikiwa mtu hawezi kusujudu kabisa, basi asitumie mto wala kitu kingine, bali asujudu kwa ishara ikiwa hana uwezo wa kusujudu moja kwa moja.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24867/حكم-السجود-على-الثوب
- Imechapishwa: 30/12/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)
Related
Kusujudu juu ya kilemba na mfano wake
Swali: Ni ipi hukumu ya kuweka ncha ya Shimaagh chini wakati wa swalah na mtu akasujudu juu yake ili mtu ajiepushe na vumbi na harufu mbaya? Jibu: Ikiwa kuna haja ya mtu kusujudu juu ya Shimaagh, Ghutrah na Mishlah basi hakuna neno. Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesema: “Tulikuwa…
In "Mambo yanayochukiza katika swalah"
Sujuud kabla au baada ya salamu inahusiana na ubora
Swali: Je, Sujuud ya kusahau inakuwa kabla au baada ya salamu? Jibu: Inahusiana na ubora tu. Lakini bora zaidi ni kwamba ikiwa mtu amesalimu huku akiwa amepunguza, basi katika hali hiyo asujudu baada ya salamu. Vivyo hivyo ikiwa amejengea juu ya dhana yake kubwa, Sujuud inakuwa baada ya salamu. Kwa…
In "Sujuud ya kusahau"
Kusujudu juu ya sifongo, godoro dogo au kitu mfano wake
Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kuingia msikiti ambao umetandikizwa sifongo juu yake? Ni ipi hukumu ya kusujudu juu ya vitu hivyo? Jibu: Hakuna neno kuswali katika msikiti huu. Lakini anaposujudu abonyeze juu ya sifongo hiyo mpaka itulizane. Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia: “Tulikuwa tukiswali pamoja na Mtume…
In "Kusujudu juu ya viungo saba"