Swali: Vipi ikiwa mtu atasujudu juu ya nguo yake?
Jibu: Haidhuru, hapana vibaya ikiwa atasujudu juu ya nguo yake.
Swali: Je, ikiwa atasujudu juu ya miiba?
Jibu: Ikiwa haiumizi, hakuna tatizo. Watu wengine wana ngozi ya paji la uso yenye ukakamavu na ikiwa haiumizi, basi hapana vibaya.
Swali: Je, inafaa kwake kuinua kichwa chake, kuondoa kitu hicho kisha arudi kwenye Sujuud?
Jibu: Ndio, ainue kichwa chake, aondoshe kile chenye kumkera, kisha aweke tena paji la uso wake chini.
Swali: Je, kusujudu juu ya mto?
Jibu: Bora zaidi kusujudu bila kitu. Ikiwa mtu hawezi kusujudu kabisa, basi asitumie mto wala kitu kingine, bali asujudu kwa ishara ikiwa hana uwezo wa kusujudu moja kwa moja.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24867/حكم-السجود-على-الثوب
- Imechapishwa: 30/12/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket