Swali: Je, ambaye amekula kitunguu saumu anaruhusiwa kuacha swalah ya mkusanyiko?
Jibu: Ni haramu kwake akila kwa sababu ya kuacha mkusanyiko. Hata hivyo hapana vibaya akila kwa sababu anahitaji au kwa lengo la matibabu.
Swali: Vipi ikiwa ndio mazowea yake?
Jibu: Asile ilihali kunamzuia kuswali na kunawakera watu, kwa sababu kufanya hivo kunaweza kuwa ni ujasiri wa kipumbavu wa kukosa swalah ya mkusanyiko.
Swali: Ijapo atakuwa nchi kavu?
Jibu: Asiswali pamoja nao, aswali peke yake.
Swali: Vipi wakikubaliana wote?
Jibu: Hapo wataswali wote, kwa sababu kila mmoja atakuwa na ugonjwa [huo wa kutoa harufu].
Swali: Lakini (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“… asiukurubie msikiti wetu.”[1]
Vipi ikiwa watakuwa nchi kavu kwenye hema na hawana msikiti?
Jibu: Lakini atawaudhi marafiki zake.
Swali: Si imepokelewa pia kuwa Malaika wanaudhika?
Jibu: Asikurubie msikiti hata kama hakuna mtu, kwa sababu Malaika wanaudhika kwa yale yanayowaudhi watu.
Swali: Je, hilo linahusu pia sigara?
Jibu: Ni kila ambacho kina harufu mbaya.
Swali: Katika Hadiyth kumetajwa kitunguu saumu na kitunguu maji. Katika kichwa cha khabari cha mlango kumetajwa: “Mlango unaozungumzia kitunguu saumu, kitunguu maji na figili.”?
Jibu: Ni mfano wake. Maana ni moja.
Swali: Bora ni yeye asubiri mpaka iondoke ile harufu kwa sababu asiwakere Malaika au aswali papohapo?
Jibu: Aswali nyumbani kwake.
Swali: Je, nyumbani kwake asubiri mpaka iondoke ile harufu?
Jibu: Hapana, apunguze ile harufu na aswali nyumbani kwake.
Swali: Vipi kuhusu ambao wametofautisha na kusema kwamba ikiwa harufu ni yenye kuenea msikiti mzima ndio mtu ambaye amekatazwa, lakini ikiwa harufu imekomeka kwake pekee…
Jibu: Hapana, harufu inamkera na inawakera walio pembeni yake. Sio lazima harufu isambae msikiti mzima… harufu inamuudhi jirani yake aliyeko kuliani na kushotoni.
Swali: Je, makusudio ni kukatazwa ile swalah inayoswaliwa sasa?
Jibu: Ni mamoja ile swalah inayoswaliwa sasa au nyenginezo muda wa kuwa bado yuko na harufu ya kitunguu saumu na kitunguu maji.
Swali: Ikiwa harufu itaendelea kwa vipindi vitano vya swalah au vipindi sita vya swalah?
Jibu: Asisogelee msikiti ijapo ni swalah za faradhi tano au sita.
Swali: Je, inamuhusu pia ambaye ana harufu mbaya ya mdomo au kikwapa?
Jibu: Ajitibishe na kutumia dawa. Ikiwa ni maradhi ajitibishe.
Swali: Makatazo ni kwa njia ya uharamu?
Jibu: Huo ndio udhahiri wa Hadiyth kwamba ni haramu.
[1] Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb”, nr. 333))
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23790/حكم-المسجد-والجماعة-لمن-به-راىحة-كريهة
- Imechapishwa: 01/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)