Swali: Ni vipi mtu atajishusha kwa mtu ambaye anafanya kiburi?
Jibu: Apambane na nafsi yake katika kujishusha.
Swali: Nakusudia kuwa ni vipi mwenye kujishusha atataamiliana na mwenye kufanya kiburi?
Jibu: Amnasihi na kumwelekeza katika kheri.
Swali: Lakini aendelee katika kunyenyekea hata pamoja na mwenye kufanya kiburi?
Jibu: Pamoja na kila mtu. Amnasihi.
Swali: Baadhi ya watu ukiwanasihi wanakwambia uiangalie nafsi yako.
Jibu: Haijalishi kitu. Mwambie naiangalia nafsi yangu na nafsi yako. Mwambie kuwa umeamrishwa jambo hilo. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
وَالْمُؤْمِنُونَ وَالْمُؤْمِنَاتُ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ ۚ يَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ
“Waumini wanaume na waumini wanawake ni marafiki wao kwa wao; wanaamrisha mema na wanakataza maovu.” (09:71)
Mwambie mimi nitaulizwa juu ya hilo.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22340/كيف-يكون-التعامل-مع-المتكبر
- Imechapishwa: 11/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)