Swali: Ni ipi hukumu ya ambaye anaacha kufunga kwa sababu ya maradhi sugu yanayomwandama sasa kwa miaka kadhaa?
Jibu: Madaktari wakithibitisha kuwa magonjwa yake hayatarajiwi kupona, ingawa Allaah ndiye mponyaji. Wakati mwingine madaktari wanathibitisha kuwa hatopona lakini baadaye akaponywa na Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Muhimu ni kwamba madaktari wakithibitisha kuwa magonjwa yake hayatarajiwi kupona, basi ni sawa akalisha chakula masikini kwa kila siku moja itayompita. Mola wetu (´Azza wa Jall) amesema:
وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ
”Kwa wale wanaoiweza lakini kwa tabu watoe fidia.”[1]
Hivo ndivo alivyokuwa akifanya Maalik wakati alipokuwa na umri wa kutoweza kufunga akawa analisha chakula masikini kwa kila siku moja iliyompita.
[1] 02:184
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 78
- Imechapishwa: 17/03/2024
Swali: Ni ipi hukumu ya ambaye anaacha kufunga kwa sababu ya maradhi sugu yanayomwandama sasa kwa miaka kadhaa?
Jibu: Madaktari wakithibitisha kuwa magonjwa yake hayatarajiwi kupona, ingawa Allaah ndiye mponyaji. Wakati mwingine madaktari wanathibitisha kuwa hatopona lakini baadaye akaponywa na Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Muhimu ni kwamba madaktari wakithibitisha kuwa magonjwa yake hayatarajiwi kupona, basi ni sawa akalisha chakula masikini kwa kila siku moja itayompita. Mola wetu (´Azza wa Jall) amesema:
وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ
”Kwa wale wanaoiweza lakini kwa tabu watoe fidia.”[1]
Hivo ndivo alivyokuwa akifanya Maalik wakati alipokuwa na umri wa kutoweza kufunga akawa analisha chakula masikini kwa kila siku moja iliyompita.
[1] 02:184
Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 78
Imechapishwa: 17/03/2024
https://firqatunnajia.com/huyu-ndiye-mgonjwa-anayetakiwa-kulisha-chakula-badala-ya-swawm/