Swali: Je, inafaa kuitikia adhaana inayotolewa kupitia redio?
Jibu: Ikiwa ni katika wakati wa swalah basi imesuniwa kuitikia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mkimsikia muadhini basi semeni mfano wa anavosema, kisha niswalieni. Kwani hakika anayeniswalia mara moja basi Allaah humswalia mara kumi. Kisha niombeeni al-Wasiylah. Hakika hiyo ni ngazi Peponi ambayo haimstahikii isipokuwa mja miongoni mwa waja wa Allaah. Natumai kuwa mimi ndiye. Ambaye ataniombea kwa Allaah al-Wasilah basi umemthubutukia uombezi wangu.”
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Atakayesema wakati wa kusikia adhaana:
اللهم رب هذه الدعوة التامة والصلاة القائمة، آت محمداً الوسيلة والفضيلة، وابعثه مقاماً محموداً الذي وعدته
“Ee Allaah, Mola wa mwito huu uliotimia, swalah iliosimama, mpe bwana wetu Muhammad, al-Wasiylah na fadhilah na mfikishe daraja yenye kusifiwa ambayo umemuuahidi” basi utamthubutukia uombezi wangu siku ya Qiyaamah.”
Ameipokea al-Bukhaariy katika “as-Swahiyh” yake.
al-Bayhaqiy (Rahimahu Allaah) amezidisha kwa cheni ya wapokezi nzuri baada ya kumaliza kusema:
الذي وعدته إنك لا تخلف الميعاد
“… ambayo umemuuahidi. Kwani hakika wewe huendi kinyume na miadi.”
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/363)
- Imechapishwa: 30/09/2021
Swali: Je, inafaa kuitikia adhaana inayotolewa kupitia redio?
Jibu: Ikiwa ni katika wakati wa swalah basi imesuniwa kuitikia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mkimsikia muadhini basi semeni mfano wa anavosema, kisha niswalieni. Kwani hakika anayeniswalia mara moja basi Allaah humswalia mara kumi. Kisha niombeeni al-Wasiylah. Hakika hiyo ni ngazi Peponi ambayo haimstahikii isipokuwa mja miongoni mwa waja wa Allaah. Natumai kuwa mimi ndiye. Ambaye ataniombea kwa Allaah al-Wasilah basi umemthubutukia uombezi wangu.”
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Atakayesema wakati wa kusikia adhaana:
اللهم رب هذه الدعوة التامة والصلاة القائمة، آت محمداً الوسيلة والفضيلة، وابعثه مقاماً محموداً الذي وعدته
“Ee Allaah, Mola wa mwito huu uliotimia, swalah iliosimama, mpe bwana wetu Muhammad, al-Wasiylah na fadhilah na mfikishe daraja yenye kusifiwa ambayo umemuuahidi” basi utamthubutukia uombezi wangu siku ya Qiyaamah.”
Ameipokea al-Bukhaariy katika “as-Swahiyh” yake.
al-Bayhaqiy (Rahimahu Allaah) amezidisha kwa cheni ya wapokezi nzuri baada ya kumaliza kusema:
الذي وعدته إنك لا تخلف الميعاد
“… ambayo umemuuahidi. Kwani hakika wewe huendi kinyume na miadi.”
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/363)
Imechapishwa: 30/09/2021
https://firqatunnajia.com/hukumu-ya-kuitikia-adhaana-inayotolewa-kwenye-redio/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)