Swali: Je, kumepokelewa chochote juu ya muda wa kisimamo cha siku ya Qiyaamah?

Jibu: Siku ambayo ni sawa na miaka elfu khamsini. Lakini, kama alivosema Allaah (Jalla wa ´Alaa), haitofika nusu ya mchana isipokuwa atakuwa amemaliza kuhukumu kati ya watu:

أَصْحَابُ الْجَنَّةِ يَوْمَئِذٍ خَيْرٌ مُّسْتَقَرًّا وَأَحْسَنُ مَقِيلًا

“Watu wa Peponi Siku hiyo wako katika makazi bora ya kutulia na mahali pazuri kabisa pa kupumzikia.”[1]

Wanazuoni wamenyofoa hukumu hapa kwamba haitofika nusu ya mchana isipokuwa atakuwa amekwishamaliza kazi.

[1] 25:24

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22724/ما-مقدار-يوم-القيامة-والموقف-فيه
  • Imechapishwa: 02/08/2023